Header Ads

Ukweli Kuhusu; Madereva wa gazeti la mwananchi wakamatwa na mirungi

Polisi mkoani Iringa wanawashikilia watu watatu wakiwamo madereva wawili wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa
tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa,
Ramadhani Mungi alisema tukio hilo
lilitokea jana saa 11 alfajiri katika kituo cha ukaguzi cha Igumbilo mkoani hapa nabaada ya ukaguzi polisi walibaini magunia mawili
ya mirungi ndani ya gari la kusafirishia magazeti ya kampuni hiyo.

Mungi alisema mirungi hiyo ilipakiwakatika eneo la Chalinze mkoani Pwani na taarifa
za awali zinaeleza kuwa ilikuwa
ikisafirishwa kwenda Zambia.

“Taarifa zinaonyesha kuwa gari hilo
liliondoka Dar es Salaam jana saa 5:00 usiku likiwa limepakia magazeti ya Mwananchi,The Citizen na Mwanaspoti, yote yakiwa yanachapishwa na Kampuni ya
Mwananchi Communications Ltd, na
ilipofika eneo la Chalinze mkoani Pwani watuhumiwa walipakia magunia hayo ya mirungi.

“Ndani ya gunia hizo kulikuwa na mabunda 302 yenye uzito wa kilo 121 ambayo gharama zake kwa sasa hazijajulikana kwa kuwa bidhaa hiyo ilikuwa inakwenda
kuuzwa nje na sisi hatujajua soko lake huko likoje,”alisema.

Mungi aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Ayubu Gwabugano (33), mkazi wa Forest jijini Mbeya, Mohamed Rwamo (27), mkazi
wa Kiluvya, Dar es Salaam ambaye alikuwa anaendesha gari hilo na mwenzake Adamu Komba (33 ),mkazi wa Mabibo, Dar es
Salaam.

Kamanda Mungi alisema usafirishaji wa mirungi kupitia Mkoa wa Iringa
umeongezeka kulinganisha na mwaka jana.

Alisemakuwa katika kipindi cha Januari hadi Novemba mwaka huu jeshi hilo limekwishakamata kilo 201 za mirungi wakati katika kipindi kama hicho mwaka jana walikamata kilo 75 pekee.

Akizungumzia tukio hilo,Mkurugenzi
Mtendaji wa MCL, Francis Nanai alisema, “Jambo hili limetushtua na kutusikitisha sana, mimi binafsi na wafanyakazi wenzangu wa MCL.

Tukio hili limefanywa na
madreva wetu wakijua wazi kwamba (1) sheria ya kampuni inazuia magari ya magazeti kubeba abiria wa aina yoyote (2)
hairuhusiwi kubeba mzigo wa aina yoyote isipokuwa magazeti ya MCL pekee. Na katika hili MCL haihusiki kwa hali yoyote ile kwani
hatujawahi, hatufanyi na hatuna mpango wa kujihusisha katika biashara yoyote haramu.

Kwa vile kosa ni la jinai, basi sheria
itachukua mkondo wake na tunaomba vyombo vya usalama vichukue hatua kali kabisa kwa wote waliohusika. Sisi MCL tutashirikiana na yeyote mwenye mapenzi
mema katika juhudi za kukomesha biashara haramu ya aina yoyote hapa nchini.

Ninanchukua fursa hii kuwapa pole
wasomaji wetu kwa usumbufu walioupata kutokana na tukio hili la kufedhehesha na ninawahakikishia kwamba jambo hili halivumiliki hapa MCL na hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya
wahusika.”


No comments

Powered by Blogger.