Header Ads

PICHA: Serengeti Fiesta Yaweka Historia Mjini Songea


Maelfu ya mashabiki wa mji wa Songea  jana ijumaa walikusanyika katika uwanja wa Majimaji mjini humo kushuhudia shoo kali ya kihistoria iliyoporomoshwa na wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini.
 
Kwa mara ya kwanza katika historia, shoo ya Serengeti Fiesta iliingia katika viunga vya mji wa songea na shoo kali zilizokonga vilivyo nyoyo za mashabiki wa mji huo mara baada ya kufanya shoo nyingine kali kwa mafanikio katika mji wa morogoro.
 
Kama ilivyo utamaduni wake wadhamini wakuu wa shoo hiyo kampuni ya bia ya Serengeti kwa kutumia kinywaji chake kikuu Serengeti Premium Lager iliwapelekea mashabiki wa mji huo wasanii nyota wanaotamba kwa sasa katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya, wengi wao wakitumbuiza katika mji huo kwa mara ya kwanza. 
 
Godzilla, TID, Linex, Mr. Blue, Madee, Stamina, Barnaba, Ney wa Mitego, Linah, Recho, Mo Music na Baraka Da Prince ni baadhi ya wasanii waliokuwa wakisubiriwa kwa hamu na wakazi Songea.
 
Mbali na shoo hiyo, shughuli nyingine iliyofanyika ni Serengeti Super Nyota diva na mshindi atapata nafasi ya kuja kushuhudia shoo ya mwisho itakayofanyika jijini Dar es salaam mwezi ujao. Ilishangaza kuona vipaji vya ajabu walivyonavyo vijana hao wa Songea.
 
Kadri jioni ilivyokuwa ikikaribia ndivyo maelfu ya mashabiki walivyoendelea kumiminika kwa kwa wingi kuja kushuhudia shoo hiyo, sehemu kubwa ya tiketi kwa ajili ya kuingia kwenye tamasha hilo ziliendelea kununuliwa mapema kwenye milango ya saa 9 jioni kabla ya shoo kuanza. 
 
Idadi ya watu waliokuja kushuhudia tamasha la burudani la  Serengeti Fiesta ilikuwa kubwa kiasi ambacho kiliwashangaza hadi waandaji wa tamasha hilo lililofanyika kwa mara ya kwanza katika hitoria yake mkoani hapo. 
 
Uanzishwaji wa screen za LED kubwa badala ya zile za kawaida zilizokuwa zikitumika hapo awali zilionekana kuvuta hisia za wakazi wa mji wa Songea ambao wengi wao waliipongeza Primetime Promotions kwa kufanya maandalizi mazuri.
 
Shoo ilidumu kwa zaidi ya masaa nane. Godzilla, TID na Madee ni baadhi ya wasanii waliokonga vilivyo nyoyo za mashabiki waliojitokeza uwanjani hapo kabla ya msanii Ney wa Mitego na Stamina kupanda jukwaani na wimbo wao walioshirikiana kuimba uitwao “Huko kwenu vipi”.
 
“Napenda kuwashukuru mashabiki wa mjini  songea kwa kujitokeza kwa wingi katika shoo hii….kiukweli ilinishangaza na nafurahi kuwa hawakutuangusha ukichukulia kigezo kwamba shoo hiyo ilikuwa ikifanyika kwa mara ya kwanza mjini hapa katika mtiririko wa shoo zake za mwaka huu za Serengeti Fiesta”…alisema Rugambo Rodney – Meneja Chapa wa kinywaji cha Serengeti Premium Lager. 
 
Kwa mwaka huu waandaaji wa tamasha hilo walichagua mikoa 18 ambayo shoo hiyo itapita na hii ni idadi kubwa ya mikoa iliyochaguliwa katika historia ya tamasha hilo, mikoa iliyoongozeka ni 3 katika ratiba za tamasha hilo, nayo ni Bukoba, Kahama na Songea.
 
Baada ya Songea, tamasha la Serengeti Fiesta 2014 litaelekea na shoo zake katika mikoa ya Mtwara, Mbeya, Dodoma, Singida likiwa na kauli mbiu yake “sambaza upendo” kabla ya kuhitimishwa rasmi jijini Dar  tarehe 18 Oktoba  ambapo wasanii wa nyumbani watapata nafasi ya kutumbuiza jukwaa moja na msanii toka Marekani T.I ambaye kwasasa anatamba na kibao chake “No mediocre”.








MPEKUZI

No comments

Powered by Blogger.