Header Ads

LEO NI WIKI MAALUM YA WATANI ENGLAND, RATIBA ZIMA IPO HAPA!!!!



PAMOJA na kuwa wikiendi hii itakuwa na mechi 10 za Ligi Kuu england kama utachukua zote za leo, kesho na keshokutwa, mbili kati ya hizo ndiyo gumzo zaidi.
Mechi mbili za watani ambazo zitapigwa wiki hii, tena siku moja na ndiyo zitakuwa gumzo zaidi.
Liverpool itakapokuwa nyumbani dhidi ya Everton wakati Arsenal watawakaribisha wapinzani wao wakubwa Tottenham. Kazi hizi ziko katika miji ya London na Liverpool.
Unaweza kuangalia mechi yoyote utakayo, lakini hizi mbili zinaweza kuwa zinabeba ujumbe mzito zaidi kwa maana ya soka, nia ya ushindi na upinzani unaotokana na historia kwa kuwa kabla, timu hizo zilikuwa ‘mwili mmoja’.
Liverpool Vs Everton
Tokea mwaka 1955 mechi hiyo imekuwa maarufu kama “The Merseyside derby”, ndiyo mechi maarufu zaidi ya watani ambayo ilianza kupigwa kwenye ligi ya England tokea msimu wa 1962–63 hadi leo.
Everton nyumbani kwao ni Goodison Park na Liverpool wako Anfield.
Kiutamaduni inaaminika ndiyo mechi ya watani yenye urafiki na upendo zaidi. Siku ya mechi watu wanakaa pamoja badala ya kila watu kuwa na upande wao.
Hii inatokana kwamba, timu hizo zilikuwa pamoja Anfield, lakini zikatengana lakini bado kila familia ya jiji la Liverpool ina watu wanaounga mkono Liverpool, wengine Everton.
LEO:
Liverpool haiko katika kumi bora, iko nafasi ya 11. Inahitaji kuanza kushinda kwani katika mechi tano imepoteza tatu na kushinda mbili, si hali nzuri. Wao Everton pia hawako poa, katika mechi tano wameshinda moja, sare mbili wamepoteza mbili, hivyo kila mmoja atataka kuinukia kwa mwenzake.
Timu             Mechi       Shinda         Sare    Poteza
Liverpool       181                71                 58       52
Everton         181                  52                58       71
Mechi inayofuata (Ferbruari 7, 2015)

Arsenal  Vs Tottenham
Kwa mara ya kwanza, Arsenal na Tottenham zilikutana Novemba 19, 1887 katika mechi ya kirafiki ambayo hata hivyo haikumalizika. Kiiza kiliingia ghafla dakika tano kabla ya mechi kwisha Spurs wakiwa wanaongoza 2-1, mwamuzi akamaliza mchezo.

Mechi ya kwanza ya mshindao wakati huo ligi hiyo ikijulikana kama daraja lwa kwanza ilikuwa desemba 4, 1909 na Arsenal ikaibuka na ushindi wa bao 1-0.
Hata hivyo utani au upinzani mkubwa rasmi ulianza mwaka 1913, baada ya Arsenal kuhamia kwenye uwanja wake ambao baadaye ulijulikana kama Highbury. Arsenal ndiyo imeonekana kutawala zaidi katika mechi walizokutana za michuano mbalimbali kuanzia Premier League, Kombe la Ligi, Kombe la FA na mechi nyingi.
LEO:
Upinzani ni mkali na ushindani utakuwa juu kwa kuwa katika mechi ngumu, Spurs wameishapoteza mbili katika mechi tano, lazima watake kushinda na Arsenal walio katika nafasi ya hawajapoteza, lakini katika mechi tano, wameshinda mbili na sare tatu, si mwendo mzuri.
Timu                  Mechi       Shinda         Sare    Poteza
Arsenal                160           67                  43           50      
Tottenham         160            50                  43           67      
Mechi inayofuata (Ferbruari 2, 2015)


Tottenham Vs Arsenal
Arsenal FC               MAFANIKIO                 Tottenham
  4                          Ushindi mfululizo                        4
10                         Mechi bila ya kupoteza              12
  3                         Mechi nyingi kila ushindi            3
14                         Mechi bila kufungwa bao             9

LEO JUMAMOSI:September 27, 2014

 
14:45
Liverpool FC Liverpool
v
Everton FC Everton
17:00
Chelsea FC Chelsea
v
Aston Villa FC Aston Villa
17:00
Crystal Palace FC Crystal Palace
v
Leicester City FC Leicester City
17:00
Hull City AFC Hull City
v
Manchester City FC Manchester City
17:00
Manchester United FC Manchester United
v
West Ham United FC West Ham United
17:00
Southampton FC Southampton
v
Queens Park Rangers FC Queens Park Rangers
17:00
Sunderland AFC Sunderland
v
Swansea City AFC Swansea City
19:30
Arsenal FC Arsenal
v
Tottenham Hotspur FC Tottenham Hotspur
 

No comments

Powered by Blogger.