REAL MADRID WATWAA TUZO, KLABU BORA YA MWAKA - ULAYA
IKIWA
kutwaa mataji ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Mfalme, maarufu
kama Copa del Rey haikutosha, Real Madrid pia imeshinda tuzo ya Klabu
Bora ya Mwaka Ulaya.
Sambamba
na mafanikio yao uwanjani, pia wametuzwa kwa programu yao ya kusaidia
jamii, kupitia mradi wa Mfuko wa Real Madrid unaohusu maendeleo na elimu
uliopo mjini El Gallinero.

Mtu wa mataji: Sergio Ramos akibusu taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya Mei mwaa huu
Pedro
López, Makamu wa Rais wa Real, na Emilio Butragueño, Mkurugenzi wa
Mahusiano wa kkabu, walipokea tuzo hizo katika sherehe zilizofanyika
mjini Geneva.
Celtic
wameshinda tuzo ya Mafanikio Bora: Tuzo ya Masoko kwa kutumia Uwanja
wao mtandao wa Wi-Fi na simu za mkononi inayorahisisha kuweka taarifa za
mechi, wakati Red Bull Salzburg wamechukua tuzo ya Best Sporting Progress.
Baada ya
kufanikiwa kubeba ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na Copa del Rey, Real
Madrid imetangazwa kuwa klabu bora ya Ulaya.
Madrid
imetangazwa kuchukua tuzo hiyo kubwa zaidi kwa klabu barani Ulaya na Chama cha
Klabu za Kulipwa Ulaya (Eca) katika hafla ya tuzo iliyofanyika mjini Geneva,
Uswiss, leo.
Tuzo hiyo
ilipokelewa na Makamu wa Rais wa Real Madrid, Pedro López na mkurugenzi wa
taasisi ya uhusiano bora ya klabu hiyo, Emilio Butragueno.
Red Bull
Salzburg ilishinda tuzo ya klabu inayochipukia kwa mafanikio ya juu na Celtic
ya Scotland ikabeba tuzo ya iliyofanikiwa zaidi kimasoko.

Post a Comment