Header Ads

REAL MADRID WATWAA TUZO, KLABU BORA YA MWAKA - ULAYA

IKIWA kutwaa mataji ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Mfalme, maarufu kama Copa del Rey haikutosha, Real Madrid pia imeshinda tuzo ya Klabu Bora ya Mwaka Ulaya.
Sambamba na mafanikio yao uwanjani, pia wametuzwa kwa programu yao ya kusaidia jamii, kupitia mradi wa Mfuko wa Real Madrid unaohusu maendeleo na elimu uliopo mjini El Gallinero.
Mtu wa mataji: Sergio Ramos akibusu taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya Mei mwaa huu
Pedro López, Makamu wa Rais wa Real, na Emilio Butragueño, Mkurugenzi wa Mahusiano wa kkabu, walipokea tuzo hizo katika sherehe zilizofanyika mjini Geneva. 
Washindi wengine wa tuzo za ECA mwaka 2014 walikuwa Celtic na Red Bull
Salzburg. 
Celtic wameshinda tuzo ya Mafanikio Bora: Tuzo ya Masoko kwa kutumia Uwanja wao mtandao wa Wi-Fi na simu za mkononi inayorahisisha kuweka taarifa za mechi, wakati Red Bull Salzburg wamechukua tuzo ya Best Sporting Progress.
Wazee wa tuzo: Real Madrid wameshinda tuzo ya 



Baada ya kufanikiwa kubeba ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na Copa del Rey, Real Madrid imetangazwa kuwa klabu bora ya Ulaya.

Madrid imetangazwa kuchukua tuzo hiyo kubwa zaidi kwa klabu barani Ulaya na Chama cha Klabu za Kulipwa Ulaya (Eca) katika hafla ya tuzo iliyofanyika mjini Geneva, Uswiss, leo.
Tuzo hiyo ilipokelewa na Makamu wa Rais wa Real Madrid, Pedro López na mkurugenzi wa taasisi ya uhusiano bora ya klabu hiyo, Emilio Butragueno.
Red Bull Salzburg ilishinda tuzo ya klabu inayochipukia kwa mafanikio ya juu na Celtic ya Scotland ikabeba tuzo ya iliyofanikiwa zaidi kimasoko.

No comments

Powered by Blogger.