Header Ads

YANGA KUVUNJA UKIMYA KUHUSU OKWI LEO


MWENYEKITI WA YANGA, YUSUF MANJI (KUSHOTO) NA KATIBU MKUU WA KLABU HIYO, BENO NJOVU.


Siku moja baada ya kujiunga na Simba huku akiwa bado na mkataba na Yanga, uongozi wa Yanga utatoa ufafanuzi kuhusiana na Emmanuel Okwi.


Yanga itatoa ufafanuzi kuhusiana na Okwi kuamua kwenda Simba.


Habari kutoka ndani ya Yanga zinaeleza uongozi wa klabu hiyo kongwe utatoa ufafanuzi kuhusiana na uamuzi wa kumsajili Okwi.

Okwi ametua Simba ikiwa ni siku chache tu baada ya Yanga kuwasilisha barua TFF ikitaka afungiwe kutokana na kukiuka kanuni.

Yanga pia iliomba ilipwe fidia ya dola 200,000 (Sh milioni 330).

Kabla ya TFF haijajibu lolote kuhusiana na suala hilo, Okwi ametua Simba.


No comments

Powered by Blogger.