Header Ads

WALINZI WA JADI SUNGUSUNGU WILAYANI KAHAMA WAJIPANGA KUMALIZA TATIZO LA MAUAJI YA VIKONGWE.



WALINZI wa Jadi "Sungusungu "wilayani Kahama,mkoani Shinyanga wameweka mkakati wa kuhakikisha wanakabiliana na wauaji wa Vikongwe kwa imani za Kishirikina ambao katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Shinyanga ni tatizo kubwa.
 
Katibu Mkuu wa Sungusungu wilaya ya Kahama,Zephania Lupambe ameyasema hayo jana kwenye maadhimisho mapya ya siku ya Sungusungu yaliyofanyika kwenye Kata ya Chona na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.
 
Hata hivyo Lupambe amesema katika kukabiliana na hali hiyo kuna changamoto nyingi ambazo ni pamoja na walinzi hao wa jadi kuwa wahusika wakubwa wa mauaji hayo,hali ambayo inachangia waharifu hao kufichwa.
 
Amesema katika matukio hayo baadhi ya walinzi hao wa jadi wamekuwa wakibainika kujihusisha na mauaji hayo,hali ambayo amewataka kuacha mara moja tabia hiyo,kwani mkakati uliopo sasa likitokea tukio la kikongwe kuuawa kuanzia kitongoji husika wanaanza kuwajibishwa.
 
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kahama,James Lembeli ameuunga mkono mpango wa sungusungu hao wa kukomesha mauaji hayo na kuwataka wakishawakamata wasijichukulie sheria mkononi ya kuwauwa na badala yake wawapeleke kwenye vyombo vya sheria.
 
Lembeli amesema mpango ni mzuri iwapo utatekelezwa kama ulivyopangwa kwakuwa wauaji wenyewe wanawafahamu na wana ishi nao   hivyo ni rahisi   kuwajua kuliko hata polisi hivyo aliwaunga mkono kwa kuwachangia Shilingi Milioni Mbili,zitakazosaidia kuimarisha mkakati huo.

No comments

Powered by Blogger.