Header Ads

MLEMAVU ATUMIA MGUU WAKE WA BANDIA KUUZA DAWA ZA KULEVYA - DAR

KIJANA mmoja ambaye ni mlemavu
wa mguu, Said Tindwa (36), mkazi wa Vijibweni Kigamboni jijini Dar,
anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kutumia mguu wake wa bandia kwa ajili ya kutunzia na kuuza dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova alisema mlemavu huyo alitiwa nguvuni Agosti 1 mwaka huu kufuatia mtego uliowekwa na jeshi hilo.

Alisema uchunguzi wa awali
unaonesha kuwa mtuhumiwa huyo
amekuwa akitumia mbinu ya kuziuza dawa hizo kwa kuzificha kwenye mguu wake wa bandia.

Aidha Kova alisema kuwa dawa
alizokuwa akiziuza mlemavu huyo ni zile za viwandani kama vile cocaine, heroin na wakati mwingine bangi.

“Katika mtego maalum uliowekwa na askari wa upelelezi ndipo mlemavu huyo alikamatwa akiuza dawa hizo kwa wateja wake baada ya kuzitoa alikozificha ambapo ni ndani ya mguu huo wa bandia” alisema Kova.

Picha (chini) Kamishna Kova akiwa kashika moja ya dawa ya kulevya huku afande Alfred akiwa kashika mguu huo wa bandia anaotumia mlemavu.

No comments

Powered by Blogger.