Header Ads

Waganga wa Jadi, Wapiga Ramli wapigwa marufuku kuokoa 'Albino'


Katika kukabilina na matukio ya mauaji na ukatwaji viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi 'Albinisim' ambayo yameanza tena kushika kasi mwishoni mwa mwaka jana serikali imepiga marufuku wapiga ramli ikiwa ni pamoja na kuunda kikosi kazi kwa ajili ya operesheni maalum ya kuwasaka watuhumiwa.

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh Mathias Chikawe ameyasema hayo jijini Dar es Salaam ambapo amekiri kuongezeka kwa matukio hayo tangu mwishoni mwa mwaka jana na kuongeza kuwa timu hiyo itaundwa na watu sita, wawili kutoka chama cha Albinisim Tanzania na wanne jeshi la polisi na wataanza na mikoa mitano ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Tabora na Geita na baadaye Sumbawanga, Kagera na Mbeya.

Akijibu maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari likiwemo la malalamiko ya ucheleweshwaji wa kesi pamoja na watuhumiwa kuachiwa bila kufikishwa mahakamani Mh Chikawe amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kudai kuwa linatokana na msongamano wa kesi zilizopo mahakamani na kuongeza kuwa kwa sasa wameanza mkakati ya kuzipa kipaumbele kesi ambazo zinaigusa jamii moja kwa moja.

Naye, Mwenyekiti wa chama cha watu wenye Albinisim nchini Bw Ernest Kimaya amesema katika kukabiliana na tatizo la ucheleweshwaji wa kesi pamoja na watu wanaoachiwa huru kwa kisingizio cha kukosa ushahidi wa kutosha chama hicho kinatafuta udhamini kutoka mataifa ya nje ili wapate fedha za kuendesha kesi kwani hadi sasa kesi zilizofanyiwa kazi ni tano tu kati ya kumi na moja.

No comments

Powered by Blogger.