Header Ads

TERRY ASAINI MKATABA MPYA CHELSEA


NAHODHA wa Chelsea, John Terry amesaini Mkatabaa mpya utakaomfanya alipwe mshahara wa Pauni 150,000 kwa wiki hadi mwishoni mwa msimu wa 2015-2016, wamesema vinara hao wa Ligi Kuu England.

Aidha, beki huyo wa kati ameichzea mechi 661 The Blues tangu acheze mara ya kwanza mwaka 1998 na kufunga idadi ya mabao 63 ambayo ni rekodi kwa beki.

Katika miaka yake 17 ya kupiga kazi Stamford Bridge, mkongwe huyo mwenye umri wa 34 ameiwezesha timu kutwaa mataji 13- la karibuni zaidi ni Kombe Ligi baada ya kufunga 2-0 Tottenham mapema mwezi huu.

No comments

Powered by Blogger.