Header Ads

BARCELONA WATIKISA KOMBE LA MFALME BAADA YA KUIPIGA BILBAO 3-1

Andres Iniesta (left) and Xavi (right) hold aloft the Copa del Rey after defeating Athletic Bilbao 3-1

TIMU ya Barcelona imetwaa taji la pili msimu huu, baada ya usiku huu kuifunga Athletic Bilbao mabao 3-1 katika fainali ya Kombe la Mfalme, maarufu kama Copa del Rey Uwanja wa Nou Camp.
Lionel Messi aliwapangua mabeki wanne kuifungia Barcelona bao zuri la kwanza dakika ya 20, kabla ya Mbrazil Neymar kufunga la pili dakika ya 36.
Nyota wa Argentina, Messi akakamilisha ushindi mnono wa Barca ambao tayari wana taji la La Liga kwa bao zuri dakika ya 74, wakati bao la kufutia machozi la Bilbao lilifungwa na Williams dakika ya 79.
Barca sasa inarudi kwenye maandalizi ya kujaribu kutwaa taji la tatu, itakapokutana na Juventus katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Kikosi cha Barcelona kilikuwa; Ter Stegen; Alves, Pique, Mascherano, Jordi Alba/Mathieu, Rakitic, Busquets, Iniesta/Xavi, Messi, Suarez/Pedro na Neymar.
Athletic Bilbao; Herrerin, Bustinza, Etxeita, Laporte, Balenziaga, San Jose, Benat/Ibai, Iraola, Rico/Iturraspe, Williams na Aduriz.


Barcelona stars pose on the pitch as they close in on a treble with only the Champions League final to play
Lionel Messi wheels away after opening the scoring with a brilliant solo effort in Barcelona's one sided victory
The Argentina phenomenon beat four Bilbao defenders to score his 57th goal of another incredible season
Neymar (centre) leaps for joy after completing an intricate passing move to double Barcelona's first-half lead
Neymar pumps his fist as Barcelona take a second step towards realising their treble dream
Barcelona team-mates congratulate Messi after their talisman steals in to score his second
Barcelona players link arms to celebrate on the pitch after claiming the King's Cup at the Nou Camp
Luis Suarez uploaded this photo to his Instagram

No comments

Powered by Blogger.