Maximo awashtukia
YANGA ipo vizuri katika safu za ulinzi na
kiungo, kilichobaki sasa kocha wake, Marcio Maximo, anaifanyia
marekebisho kwa nguvu safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Genilson
Santos ‘Jaja’ na mwenzake Mrisho Ngassa ili ifunge mabao mengi.
Katika mechi tatu za kirafiki, bosi huyo
hajaridhika na ufungaji wa wachezaji hao na anataka kuwapa
mbinu kwa haraka zaidi kabla msimu haujaanza Septemba 20. Katika mechi dhidi ya Chipukizi Yanga ilishinda bao 1-0, ikacheza na Shangani ikawachapa mabao 2-0 na kumaliza na KMKM iliowakung’uta mabao 2-0.
mbinu kwa haraka zaidi kabla msimu haujaanza Septemba 20. Katika mechi dhidi ya Chipukizi Yanga ilishinda bao 1-0, ikacheza na Shangani ikawachapa mabao 2-0 na kumaliza na KMKM iliowakung’uta mabao 2-0.
Katika mchezo dhidi ya Chipukizi, bao pekee la
Yanga lilifungwa na Jaja, huku katika mchezo na Shangani, mabao ya Yanga
yalitumbukizwa na Andrey Coutinho na Salum Telela. Mabao mawili ya
Yanga dhidi ya KMKM yalifungwa na Coutinho na Hussein Javu.
Matokeo hayo yanamaanisha Yanga ina uwezo wa
kushinda kuanzia bao moja hadi mawili, hivyo Maximo sasa anainoa safu
yake ya ushambuliaji iweze kupata mabao mengi zaidi.
Akizungumza na Mwanaspoti, Maximo alisema
anafurahi kuona safu za ulinzi na kiungo zikifanya vizuri katika kuokoa
na kuanzisha mashambulizi, lakini kuna kazi kidogo katika safu ya
ushambuliaji ambayo anataka ifunge mabao mengi.
Katika mechi tatu ilizocheza Zanzibar, Yanga imefunga jumla ya mabao matano na haikuruhusu kufungwa hata bao moja.
“Safu ya ulinzi inafanya vizuri kama ilivyo ile ya
viungo, maana katika mechi tatu tulizocheza Zanzibar hawakuruhusu bao.
Kuna kazi inatakiwa kufanywa kwa washambuliaji ili kuwaongezea makali
kidogo,” alisema.
“Siyo kwamba hawafai isipokuwa natakiwa
kuwaongezea nguvu ili tuweze kupata mabao mengi kwani inaonyesha kuna
tatizo dogo kwenye umaliziaji.”
Jana Jumatatu kwenye mazoezi ya Yanga
yaliyofanyika Uwanja wa Sekondari ya Loyola, Maximo alitumia muda mrefu
kuwaelekeza washambuliaji na viungo namna ya kupiga krosi na kuunganisha
ili kutengeneza nafasi nyingi za kufunga na kupata ushindi mkubwa
kwenye mechi.
Coutinho alionekana kuwa hodari katika kupiga
krosi kutoka upande wa kushoto kwani mara nyingi mipira yake ilifika
sehemu sahihi na washambuliaji walipiga vichwa au mabeki kuokoa.
Beki Juma Abdul alionekana mara kadhaa
akimwanzishia mipira Coutinho ambaye alikuwa akiiwahi na kisha kupiga
krosi zilizokuwa zikiingia katika eneo la hatari na kuunganishwa na
washambuliaji.
Jirani ya Coutinho alikuwepo kocha msaidizi
anayeshughulikia vijana, Shadrack Nsajigwa, ambaye alikuwa akimwelekeza
jambo Abdul namna ya kumfikishia mipira Coutinho ambaye alionekana yupo
makini muda wote.
SOURCE: MWANASPORT
SOURCE: MWANASPORT

Post a Comment