Header Ads

KUMBE HATA ULAYA YAPO: PAKA JEUSI LAKATIZA UWANJANI CAMP NOU, BARCA YAUA 3-0 LA LIGA


       Mambo hayo; Paka mweusi akikatiza Uwanja wa Camp Nou jana     BARCELONA imeanza vyema La Liga kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi
ya Elche Uwanja wa Camp Npu usiku wa kuamkia leo.
Katika mchezo huo, kiungo wa Barca Javier Mascherano alitolewa nje kwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza, kocha mpya Luis Enrique akiiongoza timu kwa mara ya kwanza, alionyesha mwanzo mzuri.
Lionel Messi kushoto akifurahia baada ya kufunga mabao mawili

Lionel Messi aliifungia Barca bao la kwanza baada ya kuwazidi ujanja mabeki sita Elche, kabla ya kinda Munir El Hadaddi kufunga la pili, mabao yote kipindi cha kwanza. 
Nyota wa Argentina, Lionel Messi alifunga bao lake la pili na la tatu la kuhitimisha ushindi wa Barca baada ya jitihada binafsi kipindi cha pili.
Paka mweusi alikatiza Uwanja wa Camp Nou mwanzoni tu mwa mchezo na kusababisha mechi isimame kwa muda ili aondoke.

No comments

Powered by Blogger.